MBEYA CITY 0-2 BIASHARA UNITED: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (VPL - 20/10/2019)
Timu ya Biashara United ya mkoani Mara imepata ushindi wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu ikiichapa Mbeya City mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Mabao ya Biashara United yamefungwa na Ally Kombo dakika ya 67 na Innocent Edwin dakika ya 90 huku timu zote zikionesha mchezo wa ushindani zikishindwa kutumia nafasi kadhaa zilizopatikana.
Baada ya mchezo huo Kocha wa Mbeya City amesema haelewi ni kwanini wachezaji wake wameshindwa kuzitumia nafasi zaidi ya tatu walizopata, lakini akaahidi kufanyia marekebisho mapungufu aliyoyaona.
Kwa upande wake Kocha wa Biashara Omary Madenge ambaye aliahidi ushindi wa mabao 3-0 amesema kilichofanya ashindwe kupata idadi hiyo ya mabao ni ubora wa Mbeya City hasa kwenye safu ya ulinzi, lakini akasisitiza kuwa alistahili kupata ushindi huo kutokana na maandalizi aliyoyafanya.