Fumo Felician: Wachezaji wengi siku hizi hawajitambui (MAKALA - TPL 2018/19)
Mchezaji wa zamani wa timu ya Pamba na Yanga Fumo Felician amesema wachezaji wengi wa soka hivi sasa hawajitambui na wanashindwa kuzitumia fursa zilizopo kwaajili ya kuitangaza nchi.
Fumo amesema laiti kama fursa zilizopo sasa, zingekuwepo enzi zao, basi Tanzania ingekuwa na sura tofauti katika soka la dunia.
Amesema wachezaji wengi siku hizi hawaigi vitu vya maana bali vitu visivyokuwa vya msingi ikiwemo mitindo ya kunyoa.
Makala hii imeangazia kwa kina historia kamili ya gwiji huyo wa soka la mkoani Mwanza na Tanzania kiujumla ambaye alivuma zaidi akiwa na timu ya Soka la Pamba FC.
Katika mahojiano haya maalum kwaajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Philip Cyprian amezungumza na Fumo mwenyewe ambaye amekumbushia mengi ya enzi zake, huku akitaja kilichoifanya Pamba iwe moto wa kuotea mbali enzi hizo na kilichoifanya Pamba ipotee kwenye ramani ya soka.
Amesema baada ya soka, hivi sasa anajishughulisha na biashara ya duka akishirikiana na mke wake.