Nataka Mbao FC imalize ligi ikiwa nafasi nne za juu – Kocha Amri Said; (MAKALA - TPL 2018/19)
Kocha mpya wa timu ya Mbao FC Amri Said amesema lengo katika klabu hiyo ni kuhakikisha inashika nafasi ya tatu au ya nne baada ya miaka mitatu endapo ataendelea kuifundisha.
Amri ameeleza lengo hilo kwenye Makala hii ambayo ni miongoni mwa Makala maalum za Ligi Kuu Tanzania Bara, zinazoangazia maandalizi ya timu mbalimbali, ambapo ameweka wazi kuwa msimu huu lengo lake ni kumaliza nafasi ya saba au ya sita.
Fuatilia mahojiano haya EXCLUSIVE, ambapo kocha huyo ameeleza pia tofauti ya timu yake ya sasa na timu alizowahi kuzifundisha ikiwemo Lipuli FC.
Amri alikuwa ni mchezaji wa zamani wa Simba, amesimulia kilichokuwa kikiipa Simba makali ya kufanya vizuri katika anga ya kimataifa huku akikumbushia jinsi Simba ilivyozitesa timu kutoka ukanda wa kiarabu zikiwemo Zamalek na Ismailia.
Kocha huyo pia amezungumzia umuhimu wa Azam TV kwenye ligi ya Tanzania huku akiweka hadharani kitu ambacho anakipenda tofauti na soka.