Tulifukia mbuzi katikati ya uwanja – Mchezaji wa zamani Singida United (MAKALA - TPL 2018/19)
Mchezaji wa zamani wa soka mkoa wa Singida James Hamis Kitila, ameichambua kwa kina hitoria ya soka mkoa wa Singida katika Makala hii maalum kwaajili ya msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kitila amesema moja ya vitu ambavyo hawezi kusahau ni wakati fulani waliwahi kuchimba katikati ya uwanja na kufukia mbuzi ili washinde mechi lakini matokeo yalikuwa tofauti na matarajio, huku Haruna Moshi akichangia kuyatibua.
Mkoa wa Singida kwa sasa una timu moja ya Singida United inayoshiriki Ligi Kuu na katika makali hii, Kitila anaichambua timu hiyo huku akieleza sababu za kushindwa kwake kupanda mapema Ligi Kuu.
Kitila pia anatoa maoni yake kuhusu timu hiyo kwa jinsi anavyoiona msimu huu, Je, anaamini itamaliza ligi ikiwa nafasi ya ngapi?
Kitila pia amekumbushia historia ya kusisimua kuhusu mawe yanayouzunguka uwanja wa Namfua.
Kwa sasa Kitila ni kiongozi wa chama cha soka mkoani humo, jina lake ni Hamis Kitila, lakini alipewa jina la utani la James.
Katika safari yake ya soka, Mzee Kitila anawataja watu kama Ally Mayay, Haruna Moshi Boban na wengineo kama watu wenye mchango katika maisha yake ya soka huku akiweka wazi historia yake katika soka.
Hii ni moja kati ya Makala nyingi za Ligi kuu ambazo huruka kupitia Azam Sports 2.