Jerry Tegete ‘akiwakaanga’ wachezaji wenzake wa Kagera Sugar (MAKALA - TPL 2018/19)
Mshambuliaji mpya wa timu ya Kagera Sugar, Jerry Tegete amechukua jukumu la kuwa mtangazaji na kuwafanyia mahijiano baadhi ya wachezaji wenzake wa Kagera, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi.
Baadhi ya wachezaji waliokumbwa na maswali ya Jerry Tegete ni Edward Christopher, Japhet Makalai, Omary Mponda na Paul Nguwai.
Wachezaji hao wamezungumzia kwa ujumla walivyojipanga na Ligi Kuu msimu huu, huku wakiongelea mazingira yalivyo ndani ya timu hiyo pamoja na maisha yao binafsi nje ya soka, bila kusahau kilichowafanya wayumbe msimu uliopita kiasi cha kupambania kutoshukia daraja.
Tegete amewagawa wachezaji hao katika makundi mawili, moja likiwa ni wachezaji wapya waliosajili msimu huu na kundi lingine ni wachezaji wenyeji waliokuwepo msimu uliopita.
Katika mahojiano haya, mshambuliaji Edward Christopher ameeleza sababu za kuifunga Simba mara kwa mara tangu aachane na klabu hiyo huku akitaja chanzo cha baadhi ya majina ya utani ambayo amekuwa akipewa.
Tazama mahojiano haya.