Kipa Singida United: Napenda sana kuhonga (MAKALA - TPL 2018/19)
Jamal Mwambeleko ndiye mtangazaji kwenye kipindi hiki, na kazi kubwa aliyofanya ni kuwahoji wachezaji wenzake kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu soka na nje ya soka ikiwemo maisha yao binafsi.
Katika mahojiano haya, kuna mchezaji mmoja amesema kuwa yeye anapenda sana kuhonga wanawake. Hebu yafuatilie kwa umakini, kisha taja jina kamili la mchezaji huyo.
Wengi wameelezea jinsi ambavyo wamejipanga kuipa timu hiyo ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku wakitaja sababu za wao kuwa mabingwa msimu huu wa 2018/19.
Pia wamezungumza kuhusu maisha yao binafsi ikiwemo ushiriki wao kwenye mitandao ya kijamii pamoja na mahusiano yao ya kimapenzi.
Baadhi ya wachezaji waliozungumza ambao asilimia kubwa ni wapya, ni pamoja na Tiba John, Rajab Zahir, Jamal Mwambeleko, Boniphace Maganga, Habib Kiyombo, Kennedy Juma, Yusuph Kagoma, David Kissu,